Kitaaluma, Askofu Dag Heward-Mills ni mwuguzi na mwanzilishi wa Umoja wa Madhehebu yatokayo Kundi la Makanisa ya Lighthouse. Umoja wa Madhehebu yatokayo Kundi la Makanisa ya Lighthouse unahusisha makanisa elfu tatu yanayoongozwa na wachungaji wenye uzoefu walioandaliwa na kufundishwa kutoka ndani. Askofu Dag Heward -Mills anasimamia kundi hili la dhehebu la kikarismatiki, ambayo yanaendelea katika katika zaidi nchi 90 katika bara la Afrika, Asia, Ulaya, Carribea, Australia, Marekani Kaskazini na Kusini.

Akiwa katika huduma zaidi ya miaka ishirini na tano, Dag Heward-Mills aliandika vitabu vingi vinavyouzika sana ikiwamo ‘Stadi ya Uongozi’, ‘Uaminifu na Ukosefu wa Uaminifu’, na ‘Kanisa Kubwa’. Anajulikana kuwa mwandishi mwenye vitabu vingi katika Afrika, akiwa na vitabu vyake vilivyotafsiriwa katika zaidi ya lugha 50 pamoja na nakala zaidi ya milioni 20 zilizochapishwa

  • Unapofikiria jina "Yuda" unafikiria usaliti na mtu aliyemfanyia Yesu uovu. Marejeo ya Yuda katika Biblia, hayakosi kuongeza kwamba alimsaliti Yesu. Je, haishangazi kutambua kwamba Yuda alikuwa rafiki wa Yesu? Yuda alikuwa mmoja wa wale waliochaguliwa. Yuda alikuwa mshiriki wa karibu wa timu hiyo. Ili kukidhi vigezo vya kuwa Yuda Iskarioti, ni lazima uwe karibu na Yesu, karibu na uongozi au uwe juu sana katika uongozi. Kifungua macho kweli! Ufichuzi huu wa hivi karibuni wa mwandishi mashuhuri, mchungaji na msemaji wa mikutano Dag Heward-Mills, utafichua kila Yuda aliye miongoni mwenu.
  • Dag Heward-Mills ni mwandishi wa vitabu vingi, ikiwemo kitabu kinachouzwa sana "Uaminifu na Ukosefu wa Uaminifu". Yeye ni mwanzilishi wa dhehebu lenye makanisa zaidi ya elfu moja linaloitwa "The Lighthouse Chapel International". (Kanisa la Kimataifa la Lighthouse). Dag Heward-Mills, mwinjilisti wa kimataifa huhudumu katika Mkutano wa Injili wa Kimataifa na Yesu Mponyaji na mikutano duniani kote. kwa taarifa zaidi, tembelea www.daghewardmills.org.
  • Unyenyekevu ni sifa muhimu ya kiroho. Watu wachache walijaribu kuandika juu ya hii sifa ya kiroho ambayo si dhahiri ila muhimu. Katika juzuu hii mpya ya kusisimua, Dag Heward-Mills alifunua aina nyingi ya kiburi zinazotatiza. Hiki Kitabu kizuri, kilichoandikwa na mwenza Mkristo anayepambana pia, kitakubariki na kukutia moyo kujenga unyenyekevu wa kitoto wa Yesu Kristo.
  • Msengenyaji ni mtu anayetoa taarifa za uongo na za kuharibu kuhusu mtu mwingine, kwa kawaida kwa lengo la kuharibu sifa ya mtu huyo. Usengenyaji mara nyingi huendeshwa na chuki na nia mbaya. Msengenyaji wa kazi ya Mungu na wa watumishi wa Mungu huwa na agenda ya kishetani ya kupunguza ushawishi na huduma ya mtumishi wa Mungu na pia kuharibu sifa ya Kanisa na watumishi wa Mungu. Katika enzi hii ya mitandao ya kijamii, usengenyaji umetumika kama silaha ya kuwaangamiza watu na kuchafua sifa zao walizojitahidi kuzijenga. Katika kitabu hiki cha kufumbua macho, utajifunza mbinu za wasengenyaji na utapata faraja katika uhakika wa hukumu ya Mungu dhidi yao. Kwa mafundisho haya kutoka kwa Dag Heward-Mills, utainuka juu ya upinzani na kuwa mhudumu wa injili asiyezuilika!
  • Watu wengi wanafamu kuhusu dhambi "nne kuu": kudanganya, kuiba, usherati na kuua. Ikiwa waweza kuuliza watu wakupe orodha ya dhambi sio kwa urahisi wao kutaja dhambi ya kusahau. Lakini Neno la Mungu liko wazi kuhusu jambo hili. Kusahau sio uadilifu! Kusahau, kukosa kukiri, kukosa kukumbuka ni dhambi mbele za Mungu.
  • "Pengine mmoja wa maadui wakubwa ambaye utawahi kukutana naye ni "mshtaki kati ya ndugu". Pokea maelekezo juu ya namna silaha hii ya mashtaka inavyotumiwa na ujifunze namna ya kuishinda, unavyosoma kitabu hiki cha kiwango cha juu, cha Dag Heward- Mills.
  •   Watu wanaokuacha wanaweza kukuharibu. hakuna kitu kinachoweza kuelezea hisia ya mfadhaiko, kuchangayikiwa na mhangaiko ambazo hushuka wakati watu wanakuacha. Kitabu hiki kimeandikwa kukusaidia kupambana na uharibifu ambao unaachiliwa wakati watu wanapokuacha. Usidanganye. Kutelekezwa au kuachwa sio la kipekee kwako na utumishi wako. Wengine wengi wameteseka na mambo sawia. Shetani alikuwa muasi wa
  • Kanisa zimejazwa na wanafiki ambao huwa wakosa ushikamanifu. Ufunguo mkuu wa shetani kwa kila wakati umekuwa udanganyifu na unafiki. Kiongozi ambaye hawezi ona ndani ya barakoa ya mnafiki atateseka kwa upofu wake. Vitisho, kufahamiana na mkanganyiko ni roho mbaya ambazo kupambana na watumishi. Wakati mwingi, watu hata hawajui nini kinachopambana nao. Kitabu hiki kitakusaidia kutambua na kupambana
  • Biblia inauliza swali hili la muhimu sana: "Ni nani awezaye kumpata mtu mwaminifu?"
Hili linaonyesha jinsi ilivyo vigumu kumpata mtu mwenye sifa ya thamani sana iitwayo “uaminifu.” Je, umewahi kujiuliza kwa nini watu wengine huanza safari yao ya Kikristo kwa ari na shauku, lakini huanguka njiani?
Kwa nini wengine huanza kwa moto wa huduma lakini huishia katika uharibifu?
  • Uasi si kosa tu - ni kosa kubwa machoni pa Mungu! Uasi ni roho inayokaidi mamlaka na kwenda kinyume na utaratibu uliowekwa na Mungu. Ni mzizi wa machafuko na unaweza kukuongoza kwenye kiza kinene cha maisha na huduma, ikiwa utairuhusu katika maisha yako! Kumbuka, uasi ulikuwa dhambi ya kwanza kuwahi kuandikwa katika Biblia! Uasi ulimchukua malaika wa nuru na kumbadilisha kuwa shetani. Hiyo ndiyo nguvu ya uasi! Ni hatari, ni yenye hila na itakuharibu ikiwa utairuhusu kuota mizizi ndani yako. Katika kitabu hiki, utagundua jinsi ya kutambua aina mbili za uasi zilizofichika na zilizo wazi ambazo zinaweza kuingilia maisha yako au huduma yako. Usichukulie kijuu juu! Viondoe miongoni mwenu!
  • "Pengine mmoja wa maadui wakubwa ambaye utawahi kukutana naye ni "mshtaki kati ya ndugu". Pokea maelekezo juu ya namna silaha hii ya mashtaka inavyotumiwa na ujifunze namna ya kuishinda, unavyosoma kitabu hiki cha kiwango cha juu, cha Dag Heward- Mills.
     
  • Yesu Kristo ndiye Nabii mkuu zaidi aliyepata kuishi! Alitabiri kwamba maumivu na makwazo yatakuja kwa kila mmoja. Maumivu na makwazo yamesababisha uharibifu mkubwa sana katika kanisa. Ni ombi langu kwamba kwa maneno haya machache utaokolewa kutoka kwa uovu na laana inayokuja kwa njia ya kwazo. Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, uwe na maonyo: kutunga vitabu vingi hakuna mwisho; na kusoma sana ni uchovu wa mwili!

Title

Go to Top